Devotionals & EncouragementSwahili Articles

Ufalme Wake Kwanza

Share
Ufalme Wake Kwanza
Share

Mathayo 6:33 (SUV): Bali utafuteni kwanza ufalme wa Mungu, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

Mungu ni Mungu wa mpangilio, na katika mpangilio Wake, kusudi huja kabla ya mahitaji mengine. Watu wengi hukimbilia “vitu” pesa, hadhi, au fursa wakitumaini kuwa vitawaletea utoshelevu. Lakini hekima ya ufalme ni tofauti “Tafuta kwanza Ufalme wake na haki yake”

Kutafuta Ufalme wa Mungu ni kuishi kusudi la Mungu, kumfuata Yeye na haki Yake kuliko vyote. Sio kupuuza mahitaji ya kila siku, bali ni kuelewa kuwa unapoweka ajenda ya Mungu mbele, kila kitu kingine huja kama Mungu alivyo kusudia.

Mafanikio ya kweli hayapatikani kwa kuangalia ni kiasi gani nilicho pata, bali kwa kiwango gani nimeweza kuwa karibu na kusudi la mbingu hapa duniani. Tunapoelekeza macho yetu kwenye kusudi la Mungu ndio njia rahisi ya kuyapa maisha yetu maana na thamani. Tutaanza kunena kwa hekima, maneno yetu yatajaa neema, tutaathiri maisha ya kizazi kinacho kuja baada yetu.

Usifanye kosa la kuanza kutafuta kwanza nyongeza kabla ya lili lililo kuu Ufalme wa Mbinguni. Mungu habariki walio upotevuni hubariki walio katika kusudi lake/mpangilio wa vipaumbele vyake ambayo ni Ufalme wake.

Shallom!

SOMO LA ZIADA: Methali 19:21; Warumi 12:2

TONO LA DHAHABU:
Ufalme unapokuwa kipaumbele chako, mbingu huyafanya maisha yako kuwa kipaumbele chake. Kusudi ni sumaku ya kuvuta vyote unavyo viitaji kutoka kwa Mungu.

OMBI:
Baba, nakushukuru kwa kunikumbusha kutafuta kwanza Ufalme Wako. Naweka chini kila tamaa isiyoambatana na kusudi lako juu ya maisha yangu. Nisaidie niishi kila siku nikilifuata moyo Wako. Ninaamini kuwa nikifanya hivyo, kila ninachohitaji kitaongezwa, kwa jina la Yesu, Amina.

Share

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles
Nguvu ya Neno la Mungu
Devotionals & EncouragementSwahili Articles

Nguvu ya Neno la Mungu

Andiko:“Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu kwa hekima yote…”...

Uwepo wa Mungu
Devotionals & EncouragementSwahili Articles

Uwepo wa Mungu

Katika safari yao kuelekea Kanaani, Musa hakutamani tu kufika kwenye nchi ya...

Kutoa kwa Imani na Moyo wa Furaha
Devotionals & EncouragementFinance & Stewardship in God’s WaySwahili Articles

Kutoa kwa Imani na Moyo wa Furaha

Mungu hathamini tu kile tunachotoa, bali moyo na imani iliyopo nyuma ya...

Nguvu ya Ukiri Sahihi
Devotionals & EncouragementSwahili Articles

Nguvu ya Ukiri Sahihi

Andiko:“Ufunuo 12:11 – Nao wakamshinda kwa damu ya Mwanakondoo na kwa neno...